MIPANGO NA MALENGO YA MWAKANI

Kama mjuavyo mwaka ndo huo unaelekea ukingoni,hatukuweza kufikia malengo tuliyojiwekea.Hii imetokana na blog yetu hii kuwa mpya na ufinyu wa muda ukizingatia imeudwa mwezi wa kumi hivyo kuwa na muda mfupi katika mwaka huu.Katika mwaka unaokuja tunategemea kuimalisha blog yetu hii ili iwe na muonekano wa kisasa kabisa,pia tunategemea kufikia malengo yetu kama tulivyo panga.Kama tulivyotangulia kusema hapo hawali,tutakuwa tukijihusisha na utafiti wa tekinologia lahisi kwa ajiri ya kutengeneza vitu mbali mbali kwa kutumia malighafi zinazopatikana katika mazingira husika.Katika kufanya hivyo tunaamini tutatengeneza nafasi nyingi za ajira kwa vijana pamoja na kutoa hamasa kwa vijana na wajasiriamali ili waweze kutumia vipaji vyao na kubuni vitu mbali mbali.
   Kwanza kabisa tutafundisha technologia ya utengenezaji wa mapambo mbalimbali yenye kuvutia pamoja na vifaa vingine vinavyotumika katika mazingira yetu kila siku.
    Ili uweze kujipatia huo ujuzi unatakiwa kujiunga kwa kutumia email yako ili tuweze kuwa tunakutumia mafunzo hayo.
   Wahi ukajiunge kama wewe ni mdadisi na unapenda kazi za utafiti na ubuni,tunaimani kuwa utapata manufaa na utaongeza kipato chako kwa kiwango kikubwa sana.
    Njoo tuzungumze,tushirikiane katika kutatua changamoto zinazotukabiri.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUBUNI NA KUENDESHA UJASILIA WENYE KUKULETEA MAFANIKIO

UJASIRIAMALI.

ujuzi katika ujasiriamali